Friday, July 29, 2011

MY PHOTOS: NASSER KIGWEANGALLAH







Photos of Mr. Nasser Kigwangallah with friends at a summit in Johannesburg, South Africa

Thursday, July 28, 2011

'MPs from Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ordered out of Parliament'


Opposition MPs walking out of the august house yesterday are: Tundu Lissu (Singida-East), Mr Godbless Lema (Arusha) and the Reverend Peter Msigwa (Iringa Urban)


THREE opposition members of parliament (MPs)from the opposition Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) were thrown out of Parliament yesterday for what the deputy speaker described as violating Parliamentary Standing Orders.

The lawmakers who were sent out of the House Chamber by deputy speaker Job Ndugai from the ruling party Chama cha Mapinduzi (CCM) during the morning session were the opposition's chief whip Tundu Lissu (Singida-East), Mr Godbless Lema (Arusha) and the Reverend Peter Msigwa (Iringa Urban).

Deputy Speaker Job Ndugai’s action brought to four the total number of Chadema MPs who have been thrown out of the House in the past two days.

On Wednesday, Mr Ezekiel Wenje (Nyamagana-Chadema) was also shown the door for disobeying orders to sit down.

Mr Ndugai said the MPs had violated Standing Order, Section 60 (2) that says an MP is not allowed to switch on his microphone to speak without permission.

The three MPs were demanding directions from the Deputy Speaker when the government chief whip, Mr William Lukuvi, said a speech by Mr Lema, the Shadow Minister for Home Affairs aimed at inciting people against their government.

Lukuvi, who is also the minister of state in the Prime Minister’s Office (Policy and Coordination), said Mr Lema’s speech amounted to incitement that was likely to jeopardise the country’s stability and also violated Standing Order, sections 64 (1) (a), (b), (f) and (g).

“We decided not to intervene while he was reading his speech,” the minister said, “because we (the government) wanted wananchi to hear what Mr Lema was saying so that they can judge for themselves.”

Mr Lukuvi identified the offending words as: “It is better we fight rather than live peacefully while we are denied our rights”; “Peace is not the absence of war but the presence of justice”; “The Arusha mayoral election was not legitimate.”

At this point, Mr Lissu intervened and asked why the deputy speaker allowed Mr Lukuvi to make a speech when, under the Standing Orders, an MP is allowed to make only a short statement when seeking the Deputy Speaker’s guidance.But Mr Ndugai ordered Mr Lissu to sit down as the Standing Orders do not allow MPs to seek the Deputy Speaker’s direction when another legislator was speaking.

Said the Deputy Speaker: “Mr Lissu, I demand that you sit down or I will take action against you.” As Mr Lissu obeyed the order, Mr Lema stood up and demanded the Deputy Speaker’s attention. He too was ordered to sit down and this annoyed Mr Msigwa, who shouted that the Deputy Speaker was favouring the government side of the august House. After Mr Msigwa calmed down, Mr Ndugai ordered the three MPs out of the Chamber for failing to obey the Chair and also violating Standing Orders.

Said Mr Ndugai: “Mr Lema and the Rev Msigwa; you have spoken without my permission hence violating Section 60 (2), so I order you to get out of the Chamber.” Although he did not specify how long the three MPs would stay away, the Standing Orders provide for suspension of up to five sessions.

'Askari wa Israeli waliwatia mbaroni wanaharakati saba'



Israeli atrocities to Palestinians unattainable



Askari wa Israeli waliwatia mbaroni wanaharakati saba waliokuwa wakishiriki katika maanadamano huko Al-Walaja, jana asubuhi.
Bwana Ala Ad-Deras, mjumbe wa kamati ya Kupinga Ukuta wa Kibaguzi alisema askari hao waliwatia mbaroni wanaharakati saba, wakiwemo wageni watano.
Ardhi ya kijiji kilichoko kaskazini mwa mji wa Bethlehem, pia iliharibiwa vibaya na uvamizi huo wa askari wa Israeli.
Askari hao mara nyingi huzua ghasia na fujo kwa wananchi bila sababu ya msingi, kitendo kilichosababisha maanadamano kuzuka huko, Ad-Deras.

Askari hao wanaripotiwa pia kuharibu ardhi kadhaa ya wanakijiji kwa kung’oa miti ya matunda na misonobari.
Bwana Awad Abu Sway, msemaji wa wizara ya kilimo alisema askari hao waliharibu barabara inayoelekea kwenye mti wa kihistoria wa mzeituni wenye umri wa miaka 5,000.
Barabara hiyo ilijengwa kwa ufadhili kutoka nje.

Wednesday, July 27, 2011

Umuhimu wa 'kazi' kwa maisha ya binadamu


Kazi ni sehemu isiyotengeka ya maisha ya mwanadamu. Allah Mtukufu ameifanya kazi kuwa ndio wasila wa mwanadamu katika kupata maisha (riziki) yake ulimwenguni hapa. Tusome huku tukitafakari. “YEYE NDIYE ALIYEFANYA ARDHI IWE INAWEZA KUTUMIKA (Kwa kila myatakayo) KWA AJILI YENU. BASI NENDENI KATIKA PANDE ZAKE ZOTE NA KULENI KATIKA RIZIKI YAKE, NA KWAKE YEYE NDIO MAREJEO (yenu nyote)” (67: 65).

Kwenda katika pande (sehemu/nchi) za ardhi hili ni suala la kushughulika na kuhangaika kwa ajili ya kutafuta maisha. Mitume wa Allah-Rehema na Amani ya Allah iwashukie – ambao ndio Waalimu wateule wa Allah kwa waja wake, pia nao walishiriki katika kufanya kazi. Hawa Allah asingeshindwa kuwaruzuku bila ya kufanya kazi. Lakini aliwataka wafanye kazi ili wawe ni mfano mwema wa kuigwa na sisi wafuasi wao. Pia ili kuonyesha kwamba kila mmoja. Hana budi kula kupitia jasho lake.

Huyu hjapa Nabii Daudi mfanyakazi:”….NA TUKAMLAINISHA CHUMA. (Tukamwambia). TENGENEZA (nguo za chuma) PANA NA UPIME VIZURI KATIKA KIUNGANISHA, NA FANYENI VITENDO VIZURI…….” (34:10-12)

Aya inatubainishia kwamba Nabiii Daudi – Amani ya Allah imshukie – alikuwa ni fundi muhunzi akitengeneza na kuuza mavazi ya chuma ambayo yalikuwa yakitumika vitani. Tena Allah, anamuagiza aifanya kazi yake hiyo kwa ufanisi mkubwa. Bwana Mtume – Rehema na Amani zimshukie analisisitiza suala hili la ufanisi kazini katika kauli yake: Hakika Allah anapenda mmoja wenu afanyapo kazi, basi aifanya kwa ukamilifu/uzuri (ufanisi) Al-baihaqiy). Ione nafasi ya kazi katika uislamu kupitia aya hii, tusome na tutafakari pamoja." NA ITAKAPOKWISHA SWALA (kuswaliwa) TAWANYIKENI KATIKA ARDHI MTAFUTE FADHILA ZA ALLAH……….” (62:10).

Nae Bwana Mtume Rehema na Amani zimmiminikie – anasema katika hadithi – Qudsi: “ Hakika Allah anasema: Ewe mja wangu wee! Utikise mkono wako nikuteremshie riziki.

Sheikh wa Al-Azhar akiri: Hosni Mubarak, alikuwa akiwalazimisha Maulamaa kuwakufurisha Mashia.


Sheikh Ahmed al- Tayyib

Ahmed al-Tayyib, Sheikh marufu wa al-Azhar amesema kuwa dikteta aliyeondolewa madarakani nchini Misri hivi karibuni, Hosni Mubarak alikuwa akiwalazimisha maulamaa wa Misri kutoa fatuwa za kuwakufurisha Waislamu wa madhehebu ya Shia kwa shabaha ya kuzusha khitilafu na ugomvi baina ya Shia na Sunni na kuuridhisha utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.

Sheikh wa al Azhar amefichua baadhi ya jinai hizo za Rais wa zamani wa Misri katika kikao chake na wanaharakati wa chama al Nasiri mjini Cairo. Sheikh Ahmed Al-Tayyib amesema:

"Hosni Mubarak alinitaka mara kadhaa nitoe fatuwa kali dhidi ya Mashia na Hizbullah ya Lebanon lakini nilikataa kufanya hivyo licha ya mashinikizo makali."

'Brazil yaipigia debe Palestina iungwe mkono na Kundi la 77 kwenye Umoja wa Mataifa'


Raisi wa zamani wa nchi ya Brazil Bwana Luiz Inácio Lula da Silva




Bi. Dilma Rousseff, raisi wa kwanza mwanamke nchini Brazil


RAISI wa zamani wa nchi ya Brazil Bwana Luiz Inácio Lula da Silva ameteuliwa kuwa mjumbe mahsusi wa nchi hiyo kufanya mazungumzo na Kundi la 77 juu ya kutambuliwa rasmi kwa taifa huru la Palestina kwenye Umoja wa Mataifa.
Brazil, kwa upande wake, tayari imekwisha itambua Palestina kama taifa huru kwa mujibu wa mipaka ya mwaka 1967 ilipofika mwezi Desemba, 2010 hivyo kuongoza njia kwa nchi zote za Amerika ya Kusini nazo kuitambua Palestina.
Nchi zingine ambazo tayari zimeonesha kuiunga mkono Palestina ni: Argentina, Bolivia, Ecuador na Chile na nchi nyingine kadhaa.
Hivi sasa Bwana Lula amejitolea kufanya mazungumzo na viongozi wa nchi zinazoendelea ili ziitambue Palestina haraka iwezekanavyo; ili nayo ipate uanachama wa 194 wa Baraza la Umoja wa Mataifa, mwezi Septemba mwaka huu.
“Lengo hasa la Brazil ni kuleta msukumo wa kisiasa ili Waisraeli na Wapalestina wafikie muafaka kwa njia za kidiplomasia.
Lakini kwa hali ilivyo hivi sasa, inaonesha kuwa mgogoro huu utazidi kuendelea hivyo kwa muda mrefu," alisema mshauri wa rais Marco Aurélio García kwa gazeti la O Estado.
Raisi wa Brazil Dilma Rousseff anatarajiwa kutoa hotuba yake kwenye kikao cha mwaka huu cha Baraza la Umoja wa Mataifa na suala la Palestina litakuwa mbele ya ajenda yake.



Bwana Nasser Kigwangallah, mwandishi wa habari mwandamizi akiwa 'busy' ofisini kwake jijini Dar es Salaam 28 Julai, 2011

Mr Nasser Kigwangallah, a senior journalist and reporter posed in this photo

Tuesday, July 26, 2011


Dr Athuman Rashid Mfutakamba, the Honourable member of Parliament for Igalula constituency in Taboa region. He has also been appointed by president Jakaya Kikwete as the deputy minister for transport. Will he deliver to the expectations of his electorates? Let's wait and see
. By Nasser Kigwangallah


Palestinian ambassador to Tanzania Dr Nasri Abu Jaish making a speech to journalists in his office in Dar es Salaam recently.
Photo: By Nasser Kigwangallah

'Rostam kumtunza mke wa Mwakiteleko'

Katika salamu za rambirambi, Kampuni ya New Habari 2006 Ltd imeahidi kumlipa mke wa marehemu Mwakiteleko mshahara ya kila mwezi kwa miaka mitano, kusomesha watoto wake wawili na watoto wa marehemu kaka yake hadi Chuo Kikuu.

Rostam Aziz, mmiliki wa New Habari Corporation, wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania, The African, Dimba nk. ameahidi kuiangalia familia ya al-marhum Danny Mwakiteleko kwa karibu zaidi, ikiwemo kuwasomesha watoto wawili wa kaka yake aliokuwa akiishi nao hadi elimu ya chuo kikuu.

Rostam alisema kuwa marehemu Mwakiteleko alikuwa msikivu, mwajibikaji na mchapa kazi na kabla ya kifo chake alikuwa akiandaa toleo maalumu la miaka 50 ya Uhuru, hivyo anastahiki kukumbukwa kwa yale yote aliyoyafanya.

Marehemu Mwakiteleko alipata ajali Jumatato iliyopita saa 4:00 usiku katika eneo la TIOT, Tabata baada ya kukonga lori kwa nyuma wakati akitokea kazini kwenda nyumbani kwake Tabata Chang'ombe, na kufanyiwa upasuaji wa kichwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) ambao mauti yalimkuta Jumamosi alfariki.

Mwili wa marehemu Mwakiteleko ulisafirishwa jana kwenda Mwakaleli Tukuyu, Mbeya ambako anatarajiwa kuzikwa leo.

Marehemu ameacha mke na watoto wawili.

Mtendaji Mkuu wa New habari 2006 Ltd, Bw. Hussein Bashe alisema mtoto wa kwanza wa marehemu Mwakiteleko anayesoma kitado cha tatu na mdogo wake anayesoma darasa la sita watapewa heshima kama baba yao alivyofanya kazi kwa uadilifu katika kampuni hiyo.
Jukwaa la wahariri katika salamu zao zilizosomwa na Bw. Manyerere Jackton zilisema marehemu ameacha funzo kubwa kwa wanahabari kujituma kwani kwa namna ya pekee anastahili kupata waombolezaji wengi kama walivyokuwa jana kutokana na tabia yake ya kupenda kazi.

Katika salamu mbalimbali zilizotolewa Waziri wa Habari, Michezo na Vijana Bwana Emmanuel Nchimbi, ambaye aliyemwakilisha Rais Kikwete katika hafla ya kuuaga mwili wa marehemu Danny Mwakiteleko alisema amesikitishwa sana na kifo hicho na akaahidi kuwa Ikulu nayo kwa upande wake, itatoa mkono wa pole kwa familia hiyo.

Wengine waliotoa rambirambi zao ni Jukwaa la Wahiriri sh. 3,320,000, CRDB sh. mil. 1, NHC sh. 700,000, PPF sh. 500,000, Jeshi la Polisi Tanzania sh. 200,000 Kamati ya Nishati na Madini sh. 500,000; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe alitoa sh. 200,000 na Sport FM ya Dodoma sh. 100,000 na TANESCO sh. 500,000.

'Peru, Ecuador kupiga kura kuunga mkono uanachama wa Palestina kwenye Umoja wa Mataifa'


Peruvian President Alan Garcia


Balozi wa Palestina nchini Peru na Ecuador, Bwana Walid Abdul Rahim, amesema kuwa nchi mbili hizi zitapiga kura kuunga mkono uanachama wa Palestina kwenye Umoja wa Mataifa mwezi Septemba, mwaka huu.
Rahim aliongeza kusema kuwa hadi sasa Peru inaitambua Palestina kama taifa huru toka mwaka 1947; nayo Ecuador inaitambua Palestina kwa mujibu wa mipaka ya mwaka 1967.
Akizungumza kwenye kikao cha pili cha mabalozi wa Palestina kinachofanyika huko Istanbul, nchini Uturuki Bwana Rahim alisema mkutano huo unafanyika ili kuweka mikakati ya pamoja juu ya suala la Palestina kujiunga na Umoja wa Mataifa mwezi Septemba mwaka huu.
Pia na kufanya jitihada za makusudi kuzishawishi nchi ambazo hazijaitambua Palestina hadi sasa kufanya hivyo.

Thursday, July 21, 2011

'Ureno yaunga mkono juhudi za taifa la Palestina kujitawala'


Spanish foreign minister M/s Trinidad Jimenez

WAZIRI wa Mambo ya Kigeni wa Ureno Bi Trinidad Jimenez amemwambia rais Mahmoud Abbas anayeitembelea nchi hiyo kuwa Madrid inaunga mkono jitihada zote za Palestina kuunda taifa lake huru.
"Waziri alionesha kufurahishwa mno na hatua zilizofikiwa na nchi mbili hizi katika kuimarisha uhusiano wa kidugu katika kipindi cha miaka mingi iliyopita na pia kuunga mkono juhudi zote zinazolenga kuundwa kwa taifa huru la Palestina," taarifa ya Wizara ya Mambo ya Kigeni imesema.
Bi. Jimenez pia alimweleza Bwana Abbas kwamba juhudi za Palestina kuungwa mkono kwenye Baraza la Umoja wa Mataifa ni haki kabisa na nchi yake itaiunga mkono Palestina katika suala hili.
Marekani imekuwa kimya katika kuunga mkono suala hili na imekuwa ikizitaka Israeli na Palestina kutochukua hatua itakayopelekea kuvurugika kwa mazungumzo ya kutafuta suluhu ya mgogoro huu.

Leopard mauls six Indian villagers







Indian locals were left horrified by an attack in which a stray Leopard pounced on six villagers in Prakash Nagar, West Bengal.
After a lengthy pursuit through the village the leopard was killed by two shots at close-range after attempts to tranquillise the startled animal failed.
Sources suggest one forest guard was critically injured while the others were hurt less seriously.

Wednesday, July 20, 2011

Muuguzi afanya ‘madudu' hospitali ya Kitete, Tabora


Kazi ya uuguzi ni ya wito, ifanyike kwa umakini ili kuokoa maisha ya wagonjwa

HOSPITALI ya Mkoa wa Tabora, Kitete, imeingia kwenye kashfa baada ya mmoja wa manesi wa zamu kudaiwa kufanya uzembe uliosababisha mzazi kujifungua na mtoto kuanguka sakafuni.
Tukio hilo la kuhuzunisha limetokea mjini Tabora juzi.
Mama Neema Godwin, (32), aliyeomba msaada wakati akijifungua na kushindikana na hivyo mtoto kuanguka sakafuni na mama kuzirai.
Akisimulia mkasa huo, Neema, mkazi wa Kata ya Chemchem, Manispaa ya Tabora alisema siku ya tukio alipatwa na uchungu na kufikia hatua ya kujifungua na kuomba nesi wa zamu ampime.
“Nilimuomba nesi huyo kuja kunipima anisaidie kwani niliona kuwa wakati umefika wa kujifungua lakini aligoma na kusema kuwa mimi muda bado mbona ni msumbufu,”
Anasema badala yake nesi huyo aliendelea na kazi zake, “Niliporudia tena kumuita alinieleza tena niache kelele na akaniambia ninyanyuke niende pale alipo haraka…niliamka na kuanza kumfuata kabla sijapiga hata hatua moja chupa ilipasuka na nikaamua kurudi kitandani.
“Nilipoona amekataa nilishitukia tu mtoto ametoka na kudondoka chini na hapo nilipiga kelele tena kwa kumwambia nesi huyo kuwa amekataa kuja na mtoto ametoka na kama atakufa hatokubali, ndipo nesi huyo aliopokuja mbio kumchukua mtoto huyo.” alisema.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Kitete, Mkoa wa Tabora, Dk Lesley Mhina alikiri kuwapo kwa tukio hilo na kubainisha tayari uchunguzi umefanyika na hatua za kinidhamu zimeanza kuchukuliwa.
“Nilipopata taarifa hizi za kinyama, niliunda tume kwani nilikuwa safarini na kubaini kuwa tukio hilo lilikuwepo na tayari wahusika wote nimewatwanga barua nina imani hatua zaidi zitachukuliwa.
“Mimi binafsi nimesikitishwa na tukio hili na nimeanza kuchukua hatua kali ili hapa hospitalini kwangu tabia hii niikomeshe, wazazi wamekuwa wakilalamika mara nyingi, nataka kukomesha zaidi isijirudie, alisema Mganga huyo.

'MGANGA WA KIENYEJI TABORA ATOWEKA NA SEHEMU ZA SIRI ZA MGONJWA WAKE'


Katika hali ambayo si ya kawaida kabisa, mganga mmoja wa kienyeji, maarufu 'sangoma' ametoweka na nyeti za mgonjwa wake wa kike baada ya kuzifyeka na kisu.
Tukio hilo lilitokea Julai 6, mwaka huu majira ya saa moja usiku katika kijiji cha Mwendakulima, huko Urambo mkoani Tabora baada ya mganga huyo kumdanganya mgonjwa wake kwamba ni lazima amchanje chale sehemu za siri ili apone, kwa kuwa alikuwa amerogwa.
Ghafla, alimkata sehemu hizo na kukimbia nazo kusikojulikana hadi sasa.
Habari za uhakika kutoka Urambo zilizothibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Liberatus Barlow, zilieleza kwamba, mwanamke huyo alifariki dunia kutokana na kuvuja damu nyingi.
Alikatwa na mganga huyo, kwa madai kuwa ya kumponya ugonjwa uliokuwa ukimsumbua kwa muda mrefu.
Juhudi za kumsaka mganga huyo zinaendelea.
Polisi wamethibitisha kumsaka mganga huyo kwa udi na uvumba ili afikishwe katika vyombo vya sheria, kwa kitendo chake hicho cha kinyama.
Kamanda Barlow ametoa wito kwa wananchi mkoani Tabora kutoa taarifa polisi kuhusu watu kama hao, ambao wanajifanya waganga kumbe ni matapeli wenye lengo la kujipatia utajiri kwa njia za haramu.

Photos of Mr. Nasser Kigwangallah's family





Tuesday, July 19, 2011

Bunge la Tanzania Dodoma


Hapa ndipo wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hukutana kutunga sheria za nchi.
Ni sehemu muhimu sana kwa maendeleo na utawala wa sheria kufuatwa hapa.

'Syria yaitambua Palestina kama taifa kwa mujibu wa mipaka ya 1967'


Syrian foreign minister Farouq al- Sharaah


DAMASCUS-- Syria imetangaza kuwa inaitambua Palestina kama nchi huru kwa mujibu wa mipaka ya mwaka inayojumuisha Ukingo wa Magharibi na Uwanda wa Gaza, makao yake makuu ni Jerusalaemu ya mashariki, taarifa kutoka wizara ya mambo ya kigeni ya nchi hiyo imesema.
Taarifa imesema: “Utambuzi huu umekuja kuhakikisha haki ya Wapalestina inapatikana kikamilifu na kwamba kuonewa kunako fanywa na majeshi ya Israeli kwa wananchi wa Palestina kunakoma mara moja.”
Imeongeza kusema kuwa Ofisi ya Chama cha Wapigania Uhuru wa Palestina (PLO) iliyoko mjini Damascus imekuzwa na kuwa ofisi kamili ya ubalozi wa Palestina.
Chama cha PLO kina mipango ya kulitaka baraza kuu la Umoja wa Mataifa kuitambua Palestina kama taifa huru kwenye kikao chake cha mwezi Septemba mwaka huu, ikiwa mazungumzo ya kutafuta suluhu ya mzozo huo itashindikana.
Hata hivyo Israeli na Marekani zinapinga mpango huu wa Palestina.
Uanachama wa Palestina kwenye umoja wa mataifa unatarajiwa kuombwa na Jumuia ya nchi za Kiarabu (Arab League.)











Photos of Mr Nasser Kigwangallah in Dar



Energy and minerals PS faces dismissal


Prime Minister Mizengo Pinda said a letter written by the Permanent Secretary in the Ministry of Energy and Minerals, Mr David Jairo, had angered him as much as it angered the MPs.

The letter, addressed to unnamed officials in the ministry soliciting donations, was read in the House by Ms Beatrice Shellukindo.

In the letter, Mr Jairo asked for a contribution of 50,000,000/- from each ministry official to make the presentation of his budget estimates a success. The PM said this was a punishable, unbecoming conduct.

The letter had requested would-be donors to send the money to the Geological Survey of Tanzania (GST) in Dodoma (Account No. 5051000068 National Microfinance Bank).
The Kilindi legislator demanded to know how the donated money would be spent.

Mr Pinda said he felt like sacking the offending permanent secretary immediately but failed to do so because he had no mandate. It is President Jakaya Kikwete who can discipline the permanent secretary as he deems fit.

"President Kikwete is on a plane to South Africa. I cannot telephone him now. But I will do so as soon as he disembarks and settles down. I will advise the president on the best cause of action," Mr Pinda told the House.